Wednesday, May 10, 2017

USIICHI KWASABABU YA UWEPO LAKINI UISHI UWEPO KWA SABABU


Tokeo la picha la quotes about positive life

Nikiwa na imani kwamba leo hii ni siku muhimu sana katika maisha yako,sina shaka kuona kwamba ndoto zako pia mwaka huu zinaenda kuvuka mipaka na kuwa zaidi ya hapa unavojiona.Lakini hili litaanza kujionesha kwa kuondoa kauli ambazo zitakuwa hazina mashiko katika maisha yako kila siku na hakikisha kwamba Hausemi SIWEZI kwamaana Mungu aliyekuumba kwa mfano wake aliweza kukuumba wewe na kukupa pumzi ya kuweza kushinda kila jambo ambalo liko mbele yako.Ukiona kwamba unasema siwezi ni kwasababu unajionea uvivu kufanya unachotaka kukifanya na ni maamuzi yako pia,lakini licha ya kusema hivyo jua kwamba kauli yako ya kwanza ndiyo sababu ya wewe kuwa kama unavojiona sasahivi kwamba kweli huwezi kufanya kitu flani.Kijana mwenzangu ambaye unapenda vitu vizuri,tena ukiona kwenye tamthilia unasema kwamba na mimi nataka kuwa na gari kama lile au nataka kuwa na nyumba kama ile.Haikatazwi kufanya hivyo wala kuwa na uhitaji wa mambo mazuri kila mmoja anapenda kuwa na vitu vizuri namna ile lakini kitu kikubwa ambacho unatakiwa kukielewa ni kutokana na huu msemo wa waswahili wanakwambia kwamba “UKIONA VINAELEA JUA VIMEUNDWA” yani kunawatu kwanza walianza kuona kuelea kwa kitu hicho kabla ya hicho kitu kuanza kuelea wakiwa na maana kwamba kama ni kitu kizuri kunawatu ambao walianza kuona uzuri wa gari,nyumba na vingine vingi ambavyo unavitamani na wewe kuwa navyo lakini walichokifanya ili kuweza kupata vitu vile kuna mambo waliamua kufanya na waliamua kujitamkia maneno ya “NAWEZA”,tena sio kwamba kuweza kifikra na kimaneno tuu lakini ilikuwa ni kuweza kifikra,kimaneno na kimatendo pia.Hapa inamaana kuna mambo ambayo waliamua kuyavunja katika ratiba zao tena yale mambo ambayo hayakuwa na umuhimu na kuamua kuweka haya mambo hata kama haikuwa tabia yao kufikiri na kutenda katika upande wa kuweza lakini walijitahidi sana kuweza kuwa kama walivyokuwa na kiu ya vile vitu ambavyo walikuwa wanahitaji katika maisha yao.

Tokeo la picha la quotes about positive life
Hapa nataka kukwambia kitu gani kijana mwenzangu? Kuwa na ndoto kubwa ni kitu sahihi sana lakini haitatusaidia kama tutakuwa na wito mkubwa ndani yetu kuweza kutimiza ndoto zetu hizi kubwa.Kama utakuwa mfuatiliaji wa makala hizi nilishawahi kusema kwamba sisi kutamani kushinda katika haya maisha haitatufanya kushinda lakini maandalizi katika kuyashinda haya maisha ndicho kitu ambacho kitatufanya sisi tuweze kushinda.Jaribu kujiangalia kwamba wewe unafanya maandalizi gani na ndoto kubwa ambazo unazo,je unalala sana na kusema kwamba nina ndoto kuwa badala ya kuanza taratibu? Au je unasubiri umalize chuo ndipo uanze kufanyia kazi kwa kisingizio kwamba hauna muda wakati kila wiki unapoteza zaidi ya masaa 10 kuangalia mpira na kupiga soga? Je unaona kwamba hauna mtaji ikiwa simu yako ikaishiwa vocha unaweza kufanya juhudi yoyote kuweza kupata vocha ya 1000/= kwa siku? Toka njee ya hili box kama kweli unandoto kubwa na hakikisha kwamba unalichoma mana ukiliacha unaweza kurudi tena kule ukisema napumzika kumbe ni kurudi moja kwa moja tena.Sisi vijana hatima yetu ni zaidi ya jinsi tutakavyosuburi ajira na kusema kwamba SIWEZI kufanya jambo flani.Tunatakiwa kujiona zaidi ya jinsi tunavojiona kwamba tunaweza kufanya jambo flani katika ofisi ya kampuni flani na sio kwenye kampuni zetu.

Maisha yako ni zaidi ya tafsiri ya changamoto ambazo zinakufanya useme SIWEZI.Mapungufu yako yasiwe kigezo cha wewe kuendelea kusema kwamba SIWEZI” – LAZARO SAMWEL

CONTACTS ; 0753616584 / 0653386586

EMAIL        ;  lazarosamweli41@gmail.com

0 comments:

Post a Comment