
Habari mwanamabadiliko mwenzangu wa karne ya 21.Lengo langu ni kuhakikisha picha iliyoko akilini mwako katika muonekano wa nega ya picha inakuwa kama picha halisia kabisa.Na hii ndiyo chachu kubwa haswa katika jamii zetu kutafuta mazuri kutengeneza taifa huru kifikra.
Tunaposema kuhusu maono kwa maana kawaida tunasema kwamba ni
"uwezo wa kuona/ndoto".Kwa maana ingine tunaweza sema kwamba maono ni
picha ambayo mtu anajenga akilini mwake na anataka kuitimiza yani kuitoa kwenye
kitu ambacho kiko kwenye hali ya mawazo kwenda katika hali ya kitu ambacho kinaonekana.Kukosa
maono kwa watu wengi mara nyingi husababishwa na watu kuishi maisha ya wakati
ambao umepita na wenye maono huishi kwa kuangalia kesho yao (future).Maono
mazuri ni yale ambayo yamejengwa katika kusudi
kwasababu huku ndiko mtu anapoweza kusonga mbele kuhakikisha kwamba
anatimiza kusudi lake.Mfano wewe moja ya kusudi lako ni kwamba unataka kujenga nyumba
na akili yako umeshaweka picha halisi ya nyumba yako itakavyokuwa na wengine
unakuta kwamba wameweka mpaka picha ya kitu ambacho wanakitaka.Siri mojawapo ya
maono ni kwamba lazima uindike kwanza ndipo tunasema kwamba haya ni maono,Sijui
kama unanielewa hapa mana hauwezi kuwa na maono alafu ukawa hujaweka mipango ya
kuhakikisha kwamba ile picha inatoka katika mawazo na kuwa kitu halisia ndo
maana waingereza wansema kwamba “There is no vision without mission”.Kama huna
maono kweli hauwezi kufanya chochote zaidi ambacho utakuwa unakifanya zaidi utakuwa
na shughuli nyingi zisizokuwa na mpangilio wowote na zikawa na matokeo ambayo sio mazuri kabisa
katika maisha yako.Unajua kunatofauti kati ya mtu kuwa na matofali lakini hajui
matofali yanatakiwa kufanyiwa nini na
ukakutana mtu mwenye matofali lakini anakwambia kwamba “bwana mimi
nataka kujenga nyumba na ramani yake ni hii” hapa mwenye maono ni Yule ambaye
anamatofali lakini anaona kitu flani njee na matofali lakini Yule mwingine
ambaye anamatofali na hajui cha kufanya hana maono yoyote pia.
Tabia mojawapo ukianza kuwa na maono ambayo yako kaika kusudi lako
huwa yanabadilisha mtu kabisaa mana hayamweki mtu kuwa kaama zamani
alivyokuwa,maonon yanamfanya mtu kuishi katika kesho yake (future).Huwezi
kusema kwamba unamaono ikiwa bado ukiiangalia kesho yako unajiona
kama ulivyo leo,hayo sio maono na kama kunakitu ambacho unasema kwamba ni maono
yako na bado ukitazamia kwa mbali zaidi unajiona kwamba utakuwa palepale hauna
budi kuachana na hayo maono mana hayo sio maoni. Siku zote ukitazamia maono
yako ambayo unayo lazima utajiona mtu mwingine kabisaa na sio kama
ulivyosasahivi,maono kwamba ukishakuwa nayo na ukaona kwa mbele yatavyoweza
kukuinua kuna mambo ambayo taratibu unaanza kuacha tena unakuwa na heshima
flani kwako mwenyewe na watu wengine pia mfano
1. Lazima utaanza kuelewa matumizi yako ya pesa yanatakiwan kuwaje
na sio kutumia pesa zako kila sehemu tena hata sehemu ambazo hazina umuhimu na
wala hazikuongezei thamani yoyote.Utaelewa hela yako inatakiwa izunguke wapi na
ikuletee kitu gani maana kwa mbalin kunakitu kizuri ambacho utakuwa unakiona
kwaajili yako.
2. Utaanza kuelewa kwamba ni marafiki wa namna gani ambao
unatakiwa kuwa nao manamara nyingine maono mtu anaweza kupata kwa kuwa n watu
wenye maono lakini ukikaa na watu ambao hawana maono kuna asilimia kubwa sana
na wewe kutokuwa na maono katika maisha yako na hatimae miaka itakuwa inapita
unaishi maisha yeleyale huku mkifarijiana na wenzako ambao pia hawana maono .Angalia muda mwingine sio kwamba maisha ni magumu,jiulize watu gani ambao
umezungukwa nao katika maish yako ya kila siku,utakuta kitu ambacho unalalamika
kwa asilimia kubwa ni tabia za marafiki zako ambao unao au ambao unatumia muda
mwingi kuwa nao.Jiulize pia inakuaje kwamba unalalamika maisha magumu alafu
kunawatu kwa mwaka wanatangazwa kuwa mamilionea au mabilionea na ni umri wako?
3. Utaanza kujua umuhimu wa muda na utaelewa umuhimu wa muda
kwenye Maono yako.Hiki ni kitu ambacho watanzania wengi tunacho na tunazani
kwamba kuwa na maisha mazuri au kutimiza maono yet ni kutumia nguvu kwa muda
ambao unautaka na utafanikiwa.Vijana wa kitanzania muda mwingine hatufanikiwi
au hatuwezi kutimiza maono ambayo tunayo kwasababu ya matumizi mabovu ya muda
haswa kwenye mitandao na pia kwenye vijiwe,inawezekana kwamba vijana wengi
wanadhani kwamba kuwa na maono makubwa lazima uwe na elimu kubwa,hapana sio
ukweli mana wewe kwenye faacebook unawezaje kujua lugha ya kingereza na haujui
hiyo lugha? Mac Zukerbertg lengo lake ni kuwaleta watu sehemu moja na kuweza
kuwasiliana kama uko nae jirani,vipi wewe kwa maono ambayo unayo ya kuwa na
ardhi,nyumba,gari na biashara nyingi unadhani utazitimiza kw kupoteza muda
sehemu ambazo sio muhimu alafu ukishamaliza ndo unapata akili ya kulalamikia
serikali? Hapana kwa hivyo hatuwezi kufika na hata hatutaweza kuwa na maono na
kuyatimiza.
4. Ukiwa na maono sio kila jambo utakuwa unafanya kwakuwa
umeambiwa kwamba kunahela. Kumbuka kwamba kufanya kia jambo unalokutana nalo
katika maisha yako ni ishara ya kujionesha kwamba hauna maono yoyote kuhusu
wewe mwenyewe.Unaweza kuuliza kwamba mbona wengine wanakuwa na kazi zaidi ya
moja na bado wanaishi na kweli sisi tunachoangalia ni kwamba kuishi maisha
ambayo ni zaidi ya kawaida. Ukiwa na maono lazimo utakuwa misimamo ambayo
umeweka katika maisha yako kuhakikisha kwamba muda wako ni wewe mwenyewe
hautumiwi vibaya lakini unajitumia kuhakikisha kwamba maono yako yanatimia.
Kuna mengi sana ambayo ningependa kusema nawe lakini hizi salamu
itakuwa ni kitu tosha ambacho kitakusaidia kuhakikisha kwamba unafungua ukurasa
mpya katika maisha yako. Usikose kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA weka oda yako kukipata.Ulikuwa nami;
Lazaro Samwel (Create Youth Mindsets)
Contacts ; 0753616584 / 0653386586
Email ; lazarosamweli41@gmail.com
0 comments:
Post a Comment