Saturday, April 22, 2017

JICHO LA TATU KWA KIJANA WA KITANZANIA


Tokeo la picha la YOUTH MTIVATION PICTURES

Karibu Mpenzi msomaji wa makala Hizi za Lazaro Samwel  nikiamini mwanzo wako wa kusoma sentensi hii ni kutaka kujua zaidi kwamba wewe kama kijana kunamambo gani ambayo huyajui na unatakiwa kuyajua ili uweze pia kuelimisha wengine baada yaw ewe mwenyewe kuweza kuelimika.Naimani mwisho wa makala hii utakuwa mtu wa tofauti na fikra tofauti pia katika maisha yako haswa kama kijana. Kwa kuanza kabisa“Kijana ni kama mbegu ambayo iko aridhini ili iweze kustawi ni lazima kila siku iweze kumwagiliwa maji,kuwekewa mbolea vizuri na kupaliliwa ili itoe mazao bora”Lazaro Samwel

Kijana wa kitanzania kukutana na changamoto za hapa na pale katika maisha yake  ni kutokana na maandalizi ambayo amepewa kuanzia kwenye familia yake,shuleni na yeye mwenyewe jinsi alivyojiongeza katika maisha yake ya ujana.Changamoto nyingi ambazo huwa zinawakumbuka vijana wa kitanzania kwa asilimia kubwa cha kwanza hatakiwi kulaumiwa kwa upande,mana mafanikio ya kijana huyu kuondokana na changamoto yanaanza toka alipokuwa mdogo na ukiangalia malezi mengi ya kitanzania ni kumtoa mtoto katika kusudi lake na kumweka katika kusudi la serikali kwamba huyu motto anatakiwa akue,aende shule,afaulu aajiriwe na aitumikie serikali.Kwanini mzazi asifanye kwamba mtoto wake anatakiwa aende shule agundue kipaji chake na ajiajiri? Utajiri wa kijana unaanza kuutenegeneza kwa kutunza muda wake toka akiwa mtoto na utaharibu maisha ya kijana kwa kuuchezea muda wake toka akiwa mdogo.Tusije na siasa kwamba ni uzembe kijana kupata ajira ila ni uzembe kwa serikali kupoteza muda wa kijana toka akiwa shuleni na imani ya kuajiriwa akaacha kuwaza kuhusu kujiajiri.Mana tukumbuke kila jambo linachukua muda na hata kujiajieri sio jambo la kuamka leo na kesho kujiajiri hapo bado tutakuwa tunatengeneza taifa bovu,kijana lazima achukue muda kujijua na kujitafakari na kujua achukue muda kujifunza nini na sio anamaliza mwaka wa 3 chuo na kiongozi anasema kwamba anashangaa kuona kijana mwenye stashahada anakosa ajira,kwanini kiongozi ushangae wakati wewe ulimwambia kwamba asome utampatia ajira na sio kwamba atajiajiri? Licha ya hivyo lakini pia hata elimu anayopewa darasani ni ya kuambiwa kwamba ukienda kufanya kazi unatakiwa kufanya hivi na sio ukienda kufungua Kampuni yako unatakiwa kufanya kitu flani namna flani.

Hii ndo Tanzania ya elimu bure na sio elimu bora, na tusipoangalia tunapoelekea kwa kubadilika kwa nyakati hizi tusishangae vijana wa Tanzania wakawa watumwa katika inchi yao kwa kutumikia watu wengine kutoka inchi zingine pia.Serikali ya Tanzania ikitaka kupunguza pia hili swala la vijana kukosa ajira isianza kwa kungangania kutengeneza viwanda ila ihakikishe kwa kizazi hichi ambacho kinakuja na hata ambacho bado kipo kwenye huu mfumo wa elimu wanajikita katika kutengeneza elimu bora ya vitendo ili vijana wawe na uhakika na maisha sio kijana anaenda shule hana vidonda vya tumbo anaondoka navyo kwasababu ya msongo wa mawazo ya nini hatma ya maisha yake mana hata alipotoka na elimu yote anajiona bado ni mtupu.Tatizo sio mbegu ila ni mpanzi.
Kama nilivyosema kwamba kijana ni kama mbegu na inatakiwa kumwagiliwa,kuwekewa mbolea lakini na kupaliliwa haya yote yakikosekana mwanzo mwisho wa siku hii mbegu haiwezi kutoka mazao ambayo tuliyatarajiwa lakini sasa tusilaumu mbegu kwanini haijatoa mazao ambayo yanatakiwa tulaumu aliyepanda mbegu lakini akashindwa kumwagilia,kuwekewa mbolea na kupalilia

Nakushukuru kwa muda wako ambao umeutumia kusoma makala lakini kunawengi ambao hawajapata chansi ya kusoma makala hii jaribu kushare nao nao wafunguke.Ulikuwa nami ;

Lazaro Samwel mtunzi na mwandishi wa kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA,kwa mawasiliano zaidi tunaweza wasiliana kwa namba hizi 0753616584 au 0653386586

2 comments:

  1. Ujumbe mzuri, na jambo ambalo tunalotakiwa kufanya sisi kama vijana ni kuachana na fikra zote ambazo zitatuondoa katika kutekeleza yaleyote ambayo tumeplan kufanya.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ni kwelii kabisaa Mr Athumani Unachosema vijana inabidi tufunguke zaidi ya sasahivi tulivyo kwamaana mambo yanapoelekea inabidi sisi wenyewe ndo tuwe mabadiliko katika inchi hii.

      Delete