Sunday, May 7, 2017

KWANINI UNASHINDWA KUTUMIA RASILIMALI ULIZOKUWA NAZO ILI UWEZE KUFANIKIWA

Tokeo la picha la quotes on how to use the resources you have
Habari mpenzi msomaji wa makala hizi za Lazaro Samwel,nikiwa naimani u mzima wa afya na unaendelea vizuri na majukumu yako ya kila siku.Napenda kukupongeza kwa kuendelea kuwa mmoja wa wafuatiliaji wazuri wa makala hizi za kila siku ambazo zimelenga kumbadilisha mtu kuanzia ndani na kujiona kwamba anaweza kufanya kitu ambacho anapaswa kukifanya katika maisha yake bila kusahau kutimia vitu ambavyo vinamzunguka kwa manufaa yake na jamii yake pia.TWENDE PAMOJA.

Ningependa kwanza kuweza kukufungua kuhusu rasilimali, Nini maana ya Rasilimali?Rasilimali inaweza kuwa watu, pesa, mashine yako, ardhi na vitu ambavyo unaweza kuvitumia kukuletea matokeo flani mazuri katika maisha yako.Inawezekana ukawa unashangaa kwamba kwamba watu wanakuaje rasilimaliila kumbuka kuna kitu kinaitwa Rasilimali watu, inaweza kuwa watu ambao umewaajiri kuhakikisha kazi yako inatendeka au watu watu unewaweka kuendesha rasilimali ingine kama mashine katika kiwanda chako au kampuni yako. Leo nitapenda kwa kifupi ili nihakikishe kwamba huu ujumbe unakufungua vizuri.

Zifuatazo ni sababu za kushidwa kutumia rasilimali zako vizuri ili uweze kufanikiwa.

1. Kuwa Na Visingizio
Hakuna kibaya kama kuwa na visingizio na ukitaka hata usione kitu flani kinadhamani weka visingizio mbele. Visingizio huwa vinabadilisha mtu macho yake kuwa kama ndo akili na akili kufungwa kuona mbele pakoje. Angalia watu wengi ambao wanavisingizo na wanahela nzuri tuu au wanamshahara mzuri tuu siku zote kuishia kuwa masikini au kuishia na maisha mabovu. Visingizio lengo lake ni kwamba kuacha kushughulikia swala lako sasahivi ukidhani kesho ndipo utaliweza kulifanya lakini inakuwa uwongo kwasababu hata kisingizio chenyewe hakijui kesho yako. Hakikisha kama unamalengo mazuri na rasilimali nzuri usiiwekee kwamba kesho utaitumia anza kuifanyia kazi. Ukiipa kesho na inawezekana kesho ilikuwa iwe na matokeo mazuri na utakuwa umepoteza thamani yake.(Hii point nitaiunganisha na point ya mwisho kulandana vizuri)

2. Kutokuwa Na mtizamo chanya kwa rasilimali ambazo zinakuzunguka.
Ubongo wako ukijaza mambo mabovu usishangae kutofanya mambo mazuri, na ukitaka kujibadilisha anza kutoa huo uchafu wa mawazo  hasi na kuanza kuweka mawazo chanya ambayo yatatokana na rasilimali ambazo unazo.
Hapa  mara nyingi watu huchukua historia ya kitu flani ambacho alisikia kwa watu wengine na kuona kama ndo yeye. Ndugu unajipoteza, kumbuka huyo ambayo umewazia kilichotoea sio hata wewe na yeye sio wewe, wewe unafamilia yako na yeye anafamilia yake kwa kifupi kila mmoja anamaisha yake na hayawezi kufanana.Sasa unaporuhusu mawazo hasi kupitia maneno ya watu nakwambia haya rasilimali ambazo unazo utazitumia vibaya zaidi hata kama zilikuwa nzuri na zingeluletea mafanikio makubwa kwako.Acha tabia ya kuwa na mawazo hasi kupitia historia ya watu wengine jiangalie kivingine kutoka na maono yako yalivyo pamoja na malengo yako kupitia rasilimali ambazo unazo.

3. Kutokuthamini Muda.
Unaweza kuwa na rasilimali za aina zote, ukawa na malengo mazuri sana lakini ukiwa hujui thamani ya muda katika kuhakikisha unatumia rasilimali zako vizuri hauwezi kufika sehemu yoyote katika maisha. Mafanikio yako hayatapimwa kwa kiwango cha rasilimali ambazo unazo ila ni kwa jinsi ulivozitumia rasilimali zako kwa muda sahihi sehemu sahihi pia.Ukiona pesa yako haifanyi chochote angali unaiendeshaje sambamba na muda? Muda ni pesa( Time is Money) Hii sehemu ni pana sana sana ila cha msingi ni kwamba ukitaka kutumia rasilimali zako vizuri hakikiha unaenda na muda na usiwe mtu wa kuairisha mambo kwa kwa kudhani kwamba mambo yanakusubiri. Ndo maana kunatofauti kati ya usafiri wa gari na usafiri wa ndege watu matajiri huwa wanatumia ndege kuokoa muda sio kwamba wanapoteza hela, hapana, wanaangalia muda kwamba mfano kutoka Mwanza mpaka dar inaweza ikawa mpaka kesho lakini nikitumia fasthet ni 45 minutes, kwahiyo unamaana kama ni kufanya biashara zako unafanya na kurudi  na hata ikiwezekana unaweza kusafiri sehemu ingine kufanya biashara ingine pia ikiwe yule mwingine bado yuko safarini.

4. Kutokuwa Na Maarifa.
Hakuna sehemu ambayo unaweza kufanya bila kuwa na maarifa.Unapoamua kuanza na kuacha visingizio. Weka maarifa kwanza katika kutumia rasilimali zako. Hakikisha kwamba jinsi inavoendelea kuitumia rasilimali yako pia unaendelea kutafuta maarifa zaidi mbele yake. Lakini kama utaamua  kuanza lakini huna maarifa utasogea mbele lakini sio kama jinsi ungekuwa na maarifa zaidi. Soma vitabu sana ukajua jinsi ya kuongoza rasilimali ulizokuwa nazo na kuzielewa vizuri zaidi kadri aiku zinavozidi kwenda.
Kuwa makini na matumizi ya rasilimali ambazo unazo na hakikisha kwamba hauzitumii kukuletea manufaa ya muda mfupi lakini hakikisha kwamba unatumia rasilimali zozote ambazo unazo kwa manufaa ya muda mrefu na jamii yako ambayo inakuzunguka.

SOMA; KWANINI UNATAKIWA KUSOMA KITABU CHA NGUZO 3 ZA MAISHA 

ASANTE SANA KWA MUDA WAKO NA MUNGU AKUBARIKI,ulikuwa nami;
LAZARO SAMWEL Mtunzi na mwandishi wa kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA .
CONTACTS ; 0753616584 / 0653386586
EMAIL         ; lazarosamweli41@gmail.com

2 comments: