Sunday, May 7, 2017

KUWA MVUMILIVU NA MAFANIKIO YAKO YATAKUJA TUU.

Tokeo la picha la QUOTES ABOUT CREATIVITY IN LIFE
Habari mpenzi msomaji wa makala za Lazaro Samweli nikiwa na imani kwamba Unaendelea vizuri na harakati za kuinua kusudi lako.Leo hii nimependa kukuandalia makala hii fupi nikiwa na imani itaenda kuongeza kitu flani katika maisha yako na utasogea mbele zaidi ya pale ambapo upo sasahivi.

Tunajua katika maisha kunamsemo mmoja ambao tunausikia sana na huwa tukiusema mara nyingi ukisema kwamba “Maisha bila ufanisi humaliza ujuzi wake” kwamba maisha bila kuonesha utofauti sio kitu na ni sawa na kuwa msindikizaji wa maisha ya wengine na hapo ndipo tunaposema kwamba mtu anaanza kujiona kama hastahili mambo mazuri bali ni mabaya tuu.Ila kumbe wewe ambae  unajiona hivyo kuna mambo ambayo unakosa uvumilivu kuyafanya uweza kujitambua na kuweka ufanisi wa kutembea katika kusudi litakalokupa maisha ambayo unayataka .Nikwambie kitu usiwe na haraka kupata vitu vizuri ikiwa hata chembe ya kusudi lako haujalitambua ni bora utumie muda mwingi kuweza kutambua ni wapi roho yako inakutuma kuelekea bila kusahau kusali sana katika harakati za namna hiyo.Najua ulidhani sitaweka kitu kwamba ni lazima usali ila nakusii bila Sala bado itakuwa ni ngumu sana kujitambua unapaswa kuwa wapi zaidi, utakuwa ni mtu wa kutangatanga huku na kule bila kuwa na sehemu husika ya kuweza kutulia.

Tunaposema kuwa na uvumilivu namaanisha nini? Kwanza kabisa naomba nianze na huu msemo mmoja ambao naimani utakuja kunielewa vizuri kwamba “Maisha ni lazima yawe na changamoto mana bila changamoto hakuna mafanikio” ndomaana tunatakiwa kuwa na uvumilivu katika mambo yetu ambayo huwa tunayafanya ili tuweze kufikia malengo yetu yenye mafanikio bila hivyo tutakuwa ni watu wa kukata tamaa kila kukicha na tusione matokeo yoyote mazuri.Kwahiyo kwenye maisha lazima tukubaliane na jambo moja kwamba katika mipango yetu yote ambayo tumejiwekea lazima tukianza kuchukua hatua cha kwanza kabisa ambacho tutakutana nacho ni changamoto ambazo ziko kwa lengo la kutupima na kama hatutakuwa na uvumilivu mafanikio tutayaona kwa mbali kuanzia pale tunapokata tamaa katika changamoto ambazo tunakutana nazo. Nimekuchorea mchoro wa pyramid kuonesha kwamba tunapoweka malengo mwazo kabisa na tukaona kama ni madogo lakini sasa tukianza kushuka chini kupata mafanikio yatu tutakutana na changamoto lakini pia ukimalizana na changamoto utakutana na mafanikio ambayo ulianza kuyapangia mipango toka muda na ukaona kama ni madogo.


Piramidi Ya Mafanikio Ni Lazima unze na;
1. Mipango ; kwamba  unataka nini,kwasababu gani unakihitaji,utakipataje,sehemu  gani unaweza kukipata,na kwa muda gani unatakiwa kukipata.
2. Changamoto; Hapa ni kwamba unapoanza kufanyia kazi malengo yako sasa kunakuwa na ufungua huu changamoto ili uweze kukukaribisha katika mazingira mapya na kukufanya uwe mzoefu na sehemu ambayo itakuwa mpya katika maisha yako.
3. Mafanikio ; Ni matokeo ya uvumilivu wako katika changamoto ambazo umepitia na sio vinginevyo.Hapa sio kila mmoja huwa anafika licha ya kuweka malengo kwasababu sio kila mmoja ambaye ni mvumilivu.

Kwa Watu wengine pia wameweza kuweka Piramidi ya Mafanikio kama ifuatavyo


Picha inayohusiana
1. Unataka kuwa na nini ikiambatana na picha ya kitu ambacho unakitaka katika maisha yako haswa yawe ni maono ya mambo ambayo yako katika kutimiza kusudi lako.Kwamba ujenge picha ya jinsi kitu ambacho unakitaka kitakavyokuwa hii itakusaidia kukuongezea kasi ya kupigana katika maisha yako mfano unataka kuwa na nyumba baada ya muda wa miaka 2 sasa lazima uwe na picha kwamba nyumba yako itakuwaje ndani na njee na ujione kama uko ndani ya hiyo nyumba pia,

2.Unatakiwa kufanya nini ili uweze kusogea karibu na maono yako yani kama ni nyumba ambayo unayo akilini mwako? unachotakiwa kufanya ni  hakikisha kwamba kunakuwa na shughuli ambazo unaziweka ili uweze kuhakikisha kwamba baada ya miaka miwili unakuwa na nyumba kweli kama ni kuweka akiba kwa kiwango flani na iwe hivyo pia.

3.Weka sasa malengo kuweza kuhakikisha kwamba unatimiza ile picha na mambo ambayo umepanga kufanya.

4. Kuwa na mikakati ya kuweza kuhakikisha kwamba unatembea katika malengo yako ambayo umeshajiwekea.


Naomba kuishia hapo naimani kuna kitu ambacho umejifunza nakupongeza sana kwa kuwa pamoja name,lakini ningependa kukupa ofa ya kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA kwa bei ya upendeleo kwa kuweza kuwa na ujasiri wa kusoma na kumaliza makala hii ya POSITIVE MIND VIBE. Ni kwa watu 10 wa mwanzo tuu ambao wamesoma makala hii ndio ambao watapata kitabu.

SOMA;KWANINI UNATAKIWA KUSOMA KITABU CHA NGUZO 3 ZA MAISHA

Ulikuwa nami LAZARO SAMWEL Mtunzi na mwandishi wa kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA.Kwa mawasiliano zaidi
CONTACTS ; 0753616584 / 0653386586
EMAIL         ; lazarosamweli41@gmail.com


0 comments:

Post a Comment