Habari mpenzi msomaji wa mtandao
huu wa Lazaro Samwel naimani u mzima wa afya na Mungu Anakusaidia katika
kupambana na shughuli zako kuhakikisha kwamba mwaka huu unakuwa mwaka wa
tofauti na miaka mingine yote.Nakupongeza kwa juhudi hizo ambazo zinaonesha kiu
ya mafanikio katika maisha yako.
Najua kichwa cha makala hii
kitakuwa kimakupa hamasa sana ya kujua
kwamba kwanini usiacha kazi yako.Najua ushaambiwa mengi kuhusu ajira lakini kwa
asilimia kubwa ni kwamba umesikia ubaya wa ajira.Nikwambia kitu kuhusu ajira
ambacho nimekuja kugundua kwamba wengi wetu tumeshindwa kuelewa.Ajira ni kama
kipaji ambacho kitakusaidia kukufikisha katika kusudi lako kama kweli utaelewa
kwamba kipaji kinaweza kupotea muda wote kama hutaweza kukinoa vizuri.Ajira sio
mbovu ila sisi wenyewe ndo wabovu katika kupokea taarifa kuhusu ajira na
kujisahau kwamba njee ya ajira tunatakiwa kutengeneza maisha ambayo yatasaidia
watoto wetu kwa baadae.Ajira huwa na mtindo mmoja ambao naomba nikikumbushe
kwamba kama hutaangalia unaweza hata kusahau familia yako na hata watoto wako
muda mwingine hata wasijue uthamani wako kama mama au baba katika familia.Hii
ndo tunasema kwamba unasahau kuhusu wewe na kukumbuka kuhusu wengine ambao
wamekupa ajira kwa masaa 18 na ukirudi nyumbani unawakumbuka watoto wako
kwa lisaa 1 tuu na kusinzia.Najua hakuna
mtu ambaye anapenda maisha ya namna hii lakini pia sio makosa ya ajira makosa
ni yako kwa kuon ajira kama ndo mwisho wa kufanya mambo yako.Huwa napenda
kutumia msemo mmoja kwamba Ukiona sehemu ambayo mtu haridhiki na kile
anachokipata jua hiko sio kiyu ambacho kinaweza kumtoa kimaisha.
Kunamambo ambayo unatakiwa
kuyafanya kabla ya kuingia kwenye ajira, mana ajira sio kitu pekee cha kukutoa
kimaisha lakini inaweza kuwa usafiri wa kukutoa sehemu moja kwenda ingine kimaisha kama kweli utaelewa
mambo yafuatayo;
1.Kuwa na mpango nje ya ajira.
Na hii ukitaka kujuan kwanini
watu wengi wanaingia kwenye ajira na hata wanalipwa mshahara mkubwa lakini
maisha hayabadiliki ni kwasababu hakuna malengo na mikakati njee ya ajira
yake.Hii ina maana hata mshahara ukiingia hajui ataupeleka wapi na
atakachokiwaza ni kuhakikisha kwamba hela anaitumia kuonesha ufahari wa njee na
kuacha kuweka hela katika mpango thabiti ambao angekuwa ameupangilia ungemfanya
kuwa mbali.Huyuhuyu mwajiriwa ndiye ambaye analalamika kuhusu ugumu wa maisha
na muda mwingi wa kufanya kazi ambao unawachosha wakati anakipato kikubwa.Ndo
maana kwa wenzetu ulaya hata kama uko kwenye ajira lakini mfanyakazi anapewa
mafunzo kuhakikisha kwamba kweli ajira ambayo anaifanya inambadilisha kweli.
Kunamuda tusiseme kwamba AJIRA mbaya ila sisi ni wabaya sana hata pindi
tunapopata ajira, mana hatutendei haki hata kile ambacho tunakipata katika kazi
zetu.
Kama unajua kwamba umeajiriwa
hakikisha mambo ambayo unayafanya hayatazidi kukutoa mshahara wako au kukutoa
hela mfukoni, wazungu wanasema kwamba DON’T BUY LIABILITIE'S BUY ASSETS AND LET ASSET'S INCREASE YOUR INCOME ,hii
niliezea kwenye kitabu Changu Cha NGUZO 3
ZA MAISHA.
Sababu 1 tuu Kwanini nakwambia
kwamba usiache ajira? Ajira hautakiwi kuiacha kwasababu ifuatayo,
1. Ajira usiiache lakini itumie
iweze kukufanya wewe mwenyewe kuacha hiyo ajira.Usitumie ajira ikufanye uendelee kuitumikia. Ila itumie
ajira uache kuajiriwa ili na wewe uajiri
wengine ambao hawajui kutumia ajira zao.Tukumbuke kitu kimoja kwamba kwa
sasahivi vijana wengi wanakimbilia kuajiriwa hii ni kwasababu hawana Mipango njee
na kuajiriwa , na kijana usikimbie ajira kama huna kitu cha kufanya.Chukua
muda kwanza kuhusu kuajiriwa na piga mahesabu kwamba wewe malengo yako ni yapi
njee na kuajiriwa alafu sasa ingia kazini lakini akilini mwako kuwa na sauti ya
kwamba unafanya ajira hiyo kuweza kuhakikisha kwamba unatimiza malengo
yako njee na ajira kupitia kipato ambacho utakuwa unakipata,achana na zile tabia za kwamba mshahara hautoshi kwahiyo ngoja nikanywe pombe niumalizie huko,huku unajipeleka pabaya.Tunasema kwamba ukiitumia ajira vizuri automatical itakuhitaji wewe uiache
uende kuendelea na kuendeleza malengo yako,ila kama hautaweza kuingia na
mipango ajira unaweza kuitumikia mpaka kustafu na maisha yasiwe yamebadilika.
Nini Maoni Yako? Weka Maoni Yako.
Nashukuru Sana Kwa Muda Wako Na Ubarikiwe Sana.Kama hujapata
kitabu Changu Cha NGUZO 3 ZA MAISHA tunaweza wasiliana nami au kubadilishana
mawazo kupitia
Lazaro Samwel
Motivational And
Inspirational Speaker
Author ; NGUZO 3 ZA MAISHA
Email ; Lazaro Samwel
Contacts ;
0753616584 – 0653386586
0 comments:
Post a Comment