![]() |
| www.lazarosamwel.com |
Huu msemo ambao leo nimependa kuuweka kama kichwa cha makala
hii ni msemo ambao naimani umeanza kuusikia kwa muda mrefu sana na inawezekana
kwamba bado unaendelea kuusikia vizuri .Nimependa kuutumia mana ni msemo
ambao unalenga maisha yetu kwa asilimia kubwa sana kwasababu ni msemo ambao kwa Upande mwingine unakukumbusha
kuhusu wajibu wako hapa duniani kama umeshasahau.Huu msemo kwa lugha ingine ni
sawa na mtu kukwambia kwamba Ukiona jambo flani kwa mwenzako limetokea kama changamoto za maisha sasa na wewe inabidi kujiandaa kwa kuona tatizo ambalo mwenzako
amelipata kama la kwako. Ukiona
mwenzako alikuwa na malengo makubwa na alishawahi kukwambia kuhusu malengo yake
lakini hakuweza kutimiza ,inabidi ujifunze kutoka kwa huyo mwenzako,kaa chini
fanya mambo yako kama kesho haitakuwepo,weka mipango na mikakati kama kesho
hauatakuwepo duniani mana kunawengi ambao Mungu amekupa chansi ya kusikiliza siku
zao lakini mwisho wa siku wao wameshindwa kuzitimiza.Inabidi ujiulize kwanini
Mungu mimi tu ameniacha kusikiliza hizi ndoto za watu ambao leo hii hawapo
duniani? Nikwambie kitu kimoja kusikiliza kwako mambo ambayo wengine wameacha
hapa duniani bila hata kutimiza sio tuu taarifa ambayo inatakiwa kukufikia, ni
taarifa ambayo inatakiwa kukutoa katika usingizi ambao unao wa kusema kwamba
kesho nitaanza kufanyia kazi maono yangu au kesho ndo nitaanza kutumia muda
wangu vizuri.
Jiulize maswali mawili matatu kwamba ulisikia mangapi kwa
rafiki yetu Malumbo Sambala Mtumishi wa Mungu na Muhamasishaji ambayo yalikuwa
makubwa sana zaidi hata ya jinsi ulivokuwa unadhani na leo hii Mungu kampemnda
zaidi? Umejiuliza pia ni mangapi Steve Jobs alikuwa anatamani kuyafanya lakini
leo hii yale maono aliyokuwa nayo ameondoka nayo? Jiulize pia ulisikia marafiki
zako wangangapi ambao walikuwa na maono makubwa lakini hawajayafikia lakini na
wewe Hutaki kutia zako maji?
Nikwambie kitu mpenzi msomaji wa makala hii ya Lazaro Samwel
,haujawahi kujiuliza kwamba kunawakati unapita sehemu na unamawazo ya kitu
flani lakini ghafla unakuata watu wanaongea ,lakini ghafla ukasikia neno moja
ambalo ndilo linakuwa kama suluhisho katika mawazo yako,au ndo linakuwa kama
jibu la kitu ambacho ulikuwa ukiwaza? Huwa
naamini Mungu hufanya mambo kwa makusudi makubwa sana.Anapokuacha usikilize
matatizo ya wengine au anapokuacha uone mahangaiko ya watu wengine sio kwamba
anakupenda sana kuliko Yule ambaye unamwona ila inawezekana anampa Yule mtu
funzo kwa kutokumsikiliza zamani na kukupa
wewe mwenyewe funzo kwa unapoelekea.Ndo maana
nakwambia kwamba MWENZAKO
AKINYOLEWA ZAKO TIA MAJI, kunavitu katika maisha havipingiki ila ndo maana
tunasema kwamba TIA MAJI.Kama
umeshagundua kipaji chako kitumie sana sasahivi hakuna muda wa kusema kesho
mana kesho inaweza isiwe kesho yako.Siongei
na vijana tuu,hata na kwa watu wazima bado una chansi kubwa sana ya
kufanya makubwa sana na wewe TIA MAJI hata kama ukimwona mtu mdogo yeye
kanyolewa. Miaka Ni Namba tuu na akili hauwezi kuisema kwamba imezeka sana
kiasi kwamba hauwezi kufanya mambo makubwa.
Nashukuru Sana Kwa Muda Wako Na Ubarikiwe Sana.Kama hujapata
kitabu Changu Cha NGUZO 3 ZA MAISHA tunaweza wasiliana nami au kubadilishana
mawazo kupitia;
Lazaro Samwel
Motivational And
Inspirational Speaker
Author ; NGUZO 3 ZA MAISHA
Email ; Lazaro Samwel
Contacts ;
0753616584 – 0653386586

0 comments:
Post a Comment