Karibu mpenzi msomaji wa makala hizi za Lazaro Samwel,nikiwa na imani unaendelea vizuri na majukumu yako ya kila siku.Leo ningependa kukupa maarifa ambayo nauhakika kama utafuata ninavyokueleza lazima ufike mbali,twende pamoja.
Unapotaka kuuza bidhaa yako usimweleze mtu kwa namna ya
bado unaumiliki wa bidhaa uliyokuwa nayo ila mweleze mtu katika hali ya
kujiona ni mmiliki wa kitu unachouza.Hakuna mtu anayependa kununuliwa
lakini kila mmoja anapenda kuwa mmiliki.
Hili
ni swali ambalo kila mmoja anajiuliza katika biashara yake. Hakuna
mjasiriamali wala mfanyabiashara ambaye anaweza kunufaika na shughuli
yoyote bila kuuza.Napoongelea kuhusu kununua umiliki na kuweza kuwa na
maamuzi juu ya kitu flani.Nikwambie kitu kimoja kwamba kila mmoja anauza
haijalishi unabiashara au huna biashara lakini lazima uwe na kitu
ambacho unauza yanaweza kuwa maneno yako au matendo yako. Nakwambia hivi
kwasababu kabla ya mtu kuchukua bidhaa yoyote kwako kwanza kabisa
lazima maneno yako yaweze kununua fikra zake kabla yeye kununua bidhaa
yako kwa hela yake ndio maana biashara nzuri ipo kwenye kujenge
mahusiano na wateja wako,hapo ndipo biashara ilipo na sio pengine.
Usiangalie hela unayoipokea sasahivi kutoka kwa mteja wako tuu lakini
angalia kujenga mahusiano mazuri na mteja wako ili upate hela nyingi
kutoka kwake kwa baadae. Ukiangalia watu wengi kwenye biashara wamesahau
hili wao ilimradi mtu kaja na kuondoka basi.
Ngoja
leo nikupe siri moja kwa ufupi haswa kwa wateja ambao unawahudumia
kwasababu watu wengi hukosa kufanya mauzo mazuri kwa kutokujali kujenga
mahusiano mazuri na wateja wao katika biashara zao. Katika makala zangu
za kipindi cha nyuma nilishawahi kusena kwamba mteja wako mmoja
amekubebea wateja wengine zaidi ya 30-50 usiowajua lakini hawa
thelathini utawapata kwa kujenga mahusiano mazuri kwasababu zifuatazo
1. Mteja wa kwanza unayemuhudumia unaweza kuwa unamjua au yeye anaweza kuwa anakujua.
2.
Mteja wako anawatu wengine ambao anawajua lakini wewe huwajui na
ukijenga nae mahusiano mazuri ataweza kukuonganisha na wale usiowajua.
3.
Wale mteja wako anaowajua ambao wewe huwajui na wenyewe wanawatu ambao
mteja wako wa kwanza hawajui na wewe huwajui lakini mahusiano yako
mazuri yanaweza kufanya kuwajua wote.
Ukiangalia
kwa ukaribu biashara nzuri na ambayo itakufanya kufika mbali ni ile
ambayo inajenga mahusiano mazuri na wateja wake.Usiridhike kuona watu
wanaondoka na wala hufanyi chochote cha kuwafanya kurudi tena haswa
kujenga nao mahusiano mazuri.
Ulikuwa nami;
Lazaro Samwel
Life Coach
0753616584
Personal Email; lazarosamweli41@gmail.com
Kwa maoni kuhusu Akili Ya Ushindi ; akiliyaushindi17@gmail com
0 comments:
Post a Comment