Kuna watu ambao wapo na wanavipawa vizuri sana lakini wanakuwa
ni wasindikizaji wa kile kitu ambacho wanacho,kuna wengine ni wanawake wazuri
nikimaanisha mke ambaye anaweza kuleta mabadiliko katika familia na ni mcha
Mungu lakini mme anamtumia kama chombo flani katika familia,kuna wanawake
wengine pia wana wanaume wazuri kitabia nikimaanisha kwamba wamemshika Mungu na
wako tayari kupigana kwaajili ya faida ya familia nzima lakini bado mke katika
familia unakuwa ni mkatisha tamaa kwa mme wake na anakuwa na roho ngumu ya
kumpa moyo mme wako katika shughuli zake
za kila siku hata kama akiwa hana kitu kama yuko kwenye mashindano wakati na
ndoa wamefunga na mmekula na kiapo kwa mungu wenu. Mwanamme au mwanamke katika
familia usisindikize kipawa cha mke wako au mme wako kwasababu tayari mko naye
kwenye ndo unatakiwa kuonesha uwepo kwa kuzidi kunawirisha kitu ambacho mwenzako
anacho na sio kukipoteza.Itakuwa ni aibu kama unakuwa katika ndoa na mwenza
wako na ndo unakuwa mdidimizaji mkubwa kwa upande wa mwenzako,hapo hauwezi
kufika hata siku moja.Kuna watu ambao wanaingia katika ndoa wakiwa na mawazo ya
kama kuna mashindano lakini kumbe ni kuonesha kukua kiumri na sio kiakili
katika swala la ndoa.Ukifunga ndoa na mwenza wako jua umefunga ndoa naye kwa kila kitu ambacho anacho na ndio maana ya
kusema kwamba mnakuwa mwili mmoja na mnakuwa kama kitu kimoja mana sifa ya kuwa kitu kimoja ni kwamba
kwanza mnakuwa na mambo flani ambayo sio ya kujificha na sio ya utofauti baina
ya mwenzako na kama mngekuwa na utofauti ambao hauna muunganiko na mwenzako
hata msingeweza kufunga na ndoa pia.
Usisindikize kitu ambacho unatakiwa kukionganisha nawe ili
uweze kuwa mbali zaidi.Mfano kwa vijana tunausemi ambao wengi wameusikia
unasema kwamba “Ujana ni maji ya moto” hatuwezi kukataa kwamba kijana ni maji
ya moto lakini unasindikizaje hayo maji yako ya moto kwa manufaa yako ya baadae
mana kunamwingine anasema kwamba ni maji ya moto akisindikizwa na maneno ya
watu,vipi wewe mwenyewe baada ya kujua kwamba Ujana kweli ni maji ya moto
umefanya jambo gani kuweza kuleta matokeo mazuri ya maandalizi ya maisha yako
ya ndoa? Au umekuwa maji ya moto ambayo hayana maarifa wala hekima ya
kujitambua na kila sehemu unaona ni kutumia hali yetu ya kuwa moto kushusha
hadhi zetu? Nafasi yako sio ya kusindikiza lakini kuungana na Yule ambaye
unawaza kumsindikiza na hapo ndipo unapoweza anza kuona mabadiliko makubwa
katika kila jambo ambalo unalifanya na mwenza wako.
Lazaro Samwel
Contacts ; 0753616584 / 0653386586
Email ; lazarosamweli41@gmail.com
Youtube ; Lazaro Samwel
Facebook; Lazaro Samwel
0 comments:
Post a Comment