Habari mpenzi msomaji wa makala hizi za Lazaro Samwel nikimini kwamba u mzima wa afya na unaendelea vizuri na majukumu yako ya kila siku.Makala hii ni kwaajili yako na sio kwaajili ya mtu mwingine mana kuchukua muda wako kuweza kusoma kitu kama hichi inamaana kunathamani flani ambayo unaitafuta au unataka kuiongeza kufika sehemu ingine tofauti na mara ya kwanza.

Imekuwa ni mara nyingi sana nikiweka msisitizo wa hili swala mana najua kwa asilimia kubwa huwa linatutokea kwa kukabidhi maisha yetu kwa watu wengine ambao wao mambo ambao ni kipao mbele kutafsiri kwa haraka ni mambo ambayo yanamchango mbaya kwa binadamu au kwawenzao hawastahili kabisa, kwanini nasema hivi? Kuna watu katika maisha yako hawapo kwaajili ya kukujenga ila kwaajili ya kuhakikisha kwamba unakuwa chini ikiwezekana hata zaidi ya uafadhali ambao wanao wao. Na hawa watu huwa na tabia ya kutafuta tafsiri ya maneno ambayo ni hasi bila hata kutafakari kama ni muhimu au sio muhimu kujua maana yake na madhara ya maana yake kama mtu atakuwa nayo.Naomba nikukumbushe kitu kwamba kila mmoja anaweza kuwa jamaa yako lakini sio kila mmoja anaweza kuwa rafiki yako, kwanini nakwambia hivi? Ni kwasababu sio kila mmoja atataka kukuona kwa tafsiri nzuri ya kutaka kukuona mbali lakini kunawengine wanakuona kwa tafsiri ya kutaka kukuona kuwa mbali sana kwa nyuma yaani uwe chini zaidi ya kawaida.
Hali hii ya maisha hauwezi kuiondoa kwa kuwaambia watu sikutaki au sitaki mambo ambayo unanifanyia, lakini kumbuka ni lazima ujue na wewe tafsiri ya maisha yako ni nini kama tafsiri ya maisha yako ni mafanikio kusaidia watu, au ni mafanikio ya kubadilisha maisha ya watu wengine inabidi sasa uishi katika tafsiri hiyo lakini ijengee misimano ya kusimama na kuonesha kwanba hakuna ambaye anaweza kukutoa njee ya mstari, hii itakusaidia kuvuta watu ambao ni sahihi katika maisha yako na wale ambao sio sahihi na misimano yako wataondoka wenyewe bila hata kuambiwa. Naimani mimi na wewe ni tafsiri ya mafanikio tena haswa mafanikio ambayo yanazalisha mafanikio kwa watu wengine. Kumbuka hizi ni salamu zangu kwako na najua kunawatu ambao unajua wakipata salamu hizi utakuwa umewaokoa,sasa naomba ushare nao ujumbe huu ili uweze kuwafikia salama.
SOMA;KWANINI UNATAKIWA KUSOMA KITABU CHA NGUZO 3 ZA MAISHA
Ulikuwa nami ;
LAZARO SAMWEL mtunzi na mwandishi wa kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA.
CONTACTS : 0753616584 / 0653386586
EMAIL ; lazarosamweli41@gmail.com
0 comments:
Post a Comment