
Karibu Mpenzi msomaji wa mtandao huu wa Lazaro Samwel katika kuhakikisha kwamba unaenda kupata maarifa ambayo yatakusaidia kubadilisha maisha yako pamoja na jamii yako kwa ujumla.
USIOGOPE KUCHEKWA KWA KUTETEA KIPAJI CHAKO KUKUPELEKA KATIKA KUSUDI LAKO - Lazaro Samwel
Katika kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA niliweza kuweka
kipengele cha tofauti kati Ya KUSUDI NA KIPAJI. Nikasema kwamba Kipaji ni Kama
Alama za barabarani Kukufikisha salama sehemu ambayo unataka. Usikose kusoma
hiyo sehemu kama Bado jitahidi kupata kitabu.
Lakini nikwambia kitu
katika safari hii ya kuweza kuhakikisha kwamba unatembea ndani ya kusudi lako
sio rahisi. Na nakusihii ujue hili wala usihofie kutambua hili. Ukiweza kujua
hili safari itakuwa nyepesi kwa kiwango flani zaidi ya kutokujua. Utapingwa
sana pindi unapoamua kuanza,utakatishwa tamaa sana mana kusimama katika kusudi
lako kitakuwa kitu kipya sana mbele ya macho na akili za watu. Kusud lako
inapoanza kulifanyia kazi wengi hawawezi kuona unachokifanya mana ufunguo wewe ndiye
ambao unao na picha ya mwisho wake Mungu atakuwa amekuonesha.
Kipaji ndugu ni kitu cha kujifunza na ukiwa nacho pia
kishikilie sana unaweza kuanza kukitumia ukashangaa unaambiwa unafanya kazi
bure au unapoteza muda,cha msingi endelea kujifunza. Kipaji huanza kwa udogo sana ila unapoongeza juhudi ndipo na
chenyewe pia kinazidi kuwa kikubwa na bora zaidi.
Nikupe mfano wa Tiger Wood alianza kucheza Golf akiwa na
miaka 3 lakini alianza kuwa maarufu na kutengeneza utajiri akiwa na miaka 20
inamaana Tiger Wood ilimchukua miaka 17 kuweza kutengeneza kitu ambacho
kimemfanya kuwa Moja kati ya wanamichezo ambao wanalipwa hela nzuri zaidi. Hapa unajifunza nini? Funzo ni kwamba
haichukui muda kidogo kupata mambo makubwa lakini itachukua muda mkubwa kupata
kitu kikubwa na sahihi katika maisha yako. Ndo maana wazungu wasema ROMA
HAIKUJENGWA KWA SIKU MOJA.Cha msingi ni kuendelea kupigana tu.Kipaji chako
kinaweza kuwa katika mapishi na ndo umeanza my friend kama hapo ndipo roho,
akili na nafsi yako ipo jifunze zaidi alafu songa mbele matokeo hayaji haraka
taratibu utakuja kuyaona, kama ni mwandishi andika sana hata kama huna hela ya
kutoa kitabu kunasiku utakuja kuona umuhimu wake usisahau kuongeza maarifa ya kuandika kitu
cha tofauti zaidi na ambacho kitakuwa historia na kuacha alama katika akili za
watu, kama wewe ni muhamasishaji isihofu kwanini hujawa na mafanikio au
huonekani kwenye runinga ila endelea kukuza kipaji chako na fanya kwa usahihi
kunasiku utaitwa na wewe kutengeneza kipindi chako na watakulipa, kama wewe ni
mkulima inaweza ikawa ndo usafiri wa kukufikisha katika kusudi lako kama hiyo sehemu ndipo akili,nafsi na mwili
wako imedhamiria kufanya usiofie unapopata changamoto mana hapo ndipo mafanikio
yanapoanza kuonekana.
Jua ulimwengu unamengi hata kama ukiamua kufanya jema. Cha
msingi jaza ubongo wako kwa vitu sahihi kukufikisha katika kusudi lako.Naamini
safari ya kusudi lako lazima mkono wa Mungu utakuwepo tuu kuweza kukuongoza
mana ndipo alipokuweka wewe hapo na sio pengine. Kitabu cha NGUZO 3 ZA MAISHA
niliandika sehemu kuhusu KUSUDI kwamba Mungu Hawezi kukubariki Sehemu Ambayo
hajakuumba uwepo Hii ni ikiwa unaishi ndani ya KUSUDI la watu
wengine. Acha uteseke kwa kuchekwa, kusemwa, kusengenywa kwa kutaka mafanikio kupitia kusudi lako hata kwa miaka
10 ili uje ufurahi kwa miaka ambayo imebaki ya maisha yako hapa duniani.
@Lazaro Samwel
Motivational And Inspirational Speaker
Email ; lazarosamweli41@gmail.com
contacts ; 0753616584 /0653386586
0 comments:
Post a Comment