
Habari mpenzi msomaji wa mtandao wa Lazaro Samwel,natumaini u mzima wa afya na unaendelea vizuri na majukumu yako ya kila siku.Najua wewe ni mjasiriamali au mfanyabiashara kwa namna moja ama nyingine na makala hii ya leo ni kwaajii ya kukufanya wewe kuwa mpya katika biashara yako ambayo unaifanya,twende pamoja.
Kutoka na utafiti uliofanywa na shirika binafsi linaloitwa Bloombery ambalo linamilikiwa na mtu mmoja anaitwa Michael Bloombery kutoka marekani kuhusu Biashara Ndogondogo lilipata majibu yafutayo; 80% ya biashara ndogo hufa ndani ya mwaka mmoja zinapoanzishwa yani kwamba katika biashara ndogondogo 10 ambazo huanzishwa 8 hufa mapema ndani ya mwaka mmoja na 2 huendelea vizuri. Hata Tanzania watu wengi sana wanapenda biashara na wanapenda kuanzisha biashara zao nje ya ajira lakini kunamambo ambayo hawayajui ndio maana wengi utakuta hawafanikiwi katika hizi biashara. Katika kitabu hiki ningependa kukufungua kuweza kuelewa ni mambo gani ambayo unayakosa ili biashara yako kusonga mbele zaidi na kukuletea matokeo mazuri.
Zifuatazo ni sababu ambazo zinafanya biashara ndogo kufa
mapema pale mtu anapoamua kuianzisha.
1. Mtu kuwa na uwoga
wa kushindwa.
Hili ni swala ambalo kila mfanyabiashara anakuwa nalo na ndo
maana wengi hawafiki mbali kwasababu biashara anaiwekea mawazo ambayo ni butu.
Tukumbuke kwamba kama utakiwazia kitu
kwa ubaya lazima kunasiku kitageuka na kuwa kama jinsi ulivyokuwa ukikiwazia.Ni
sawa na biashara yako kwamba uliamua mwenyewe kwa uzuri kuifanya lakini bado
moyoni mwako unaiwazia kuishindwa kumbuka hiyo tabia ambayo unakuwa nayo ya
kuiwazia kwamba utaishindwa itakufanya kwanza ufanye biashara yako vibaya na
utaanza kujipa maneno ya uongo kwamba ulijua itakuwa hivyo, hapana wewe ndiye
ambae umesababisha mpaka ikawa hivo. Kwa kukushauri ukiona kitu kama hichi
kinakuja katika kufanya biashara yako, ikatae kabisa na usiipe nafasi katika
kuiwazia kabisaa katika akili yako mana unanguvu zaidi ya kushindwa katika
biashara yako. Na ukiona kunakisababishi cha kukufanya wewe kuona kama utanguka
katika biashara yako kaa nacho mbali hata kama ni ndugu au rafiki yako.
Mark Twain aliwahi kusema kwamba “Jiweke mbali na watu ambao wanajaribu kudogosha malengo yako/Ndoto
zako.Watu wadogo hufanya hivyo,lakini wale wakubwa watakufanya kuona kweli na
wewe unaweza kuwa mkubwa”
2. Kukosa maono
katika biashara yako.
Picha ambayo unaijenga kuhusu biashara yako ni kama nguvu
ambayo unajitengenezea kuhakikisha kwamba unafika. Ila kumbuka kwamba maono
mazuri ni yale ambayo yanaambatana na Mikakati na malengo ya jinsi ya kuweza
kuhakikisha kwamba kweli kitu kinaonekana. Yogi Berra aliwahi kusema kwamba “kama huweki malengo, usilaumu kwanini
huyafikii”.
Hakuna kitu ambacho kinaweza kumfanya mtu kufanya biashara
yake kwa juhudi kama picha ambayo ameijenga kwa baadae jinsi biashara yake
itakavokuwa.Ukiwa maono makubwa lazima utaweka juhudi kubwa na ukiwa na Maono
madogo lazima utakuwa na juhudu ndogo mana haikutishi kuyatimiza ila utakuwa
unaona kwamba hata kesho utaweza kuyatimiza.
3.Kuwa na kiu ya pesa
badala ya kuwa na kiu ya kuongeza thamani katika biashara yako kwanza.
Huwa napenda sana kusema kwamba hakuna kitu kizuri tukiwa
tunaanzisha biashara zetu hakuna kitu muhimu kama kuondoa kiu ya shidah zetu
kwanza katika pesa na kuangalia kuitengeneza biaahara zetu vizuri zaidi. Mana
biashara ndiyo ambayo itakupatia hela ambayo itakusaidia kutatua matatizo yako
na kuweza kukuhakikishia inakusaidia katika mambo mengine muhimu. Wengi huwa
tunasahau biashara tukishapata faida kidogo kwenye biashara.Naimani umeshawai
kuona watu wakifungua sehemu ya kula mwanzoni huanza kupika chakula kizuri,
kadri siku zinavyozidi kwenda na kupata faida kwa wateja kuongezeka wanaanza
kupika chakula kibovu na hawajali tena wateja kama mwanzo.Mwishi wa siku
atasema kwamba biashara yake imelogwa ila sio kwamba biashara imelogwa ila yeye
ndo mchawi wa kusababisha mpaka biashara yake kufa.
4.Kukosa Maarifa
Biashara hufa mapema ukikosa maarifa.Na biaahara kuwa ngumu
ni kukosa maarifa. Tafuta maarifa juu ya biashara yako kuondoa giza ambalo liko
ndani ya biashara yako. Tafuta maarifa juu ya kutengeneza masoko sio Tanzania
tuu dunia nzime,kujua jinsi ya kutengeneza wateja wa kudumu katika biashara
yako, pia jitahidi sana kutafuta maarifa kujua jinsi unavyoweza kuleta
mabadiliko ya biashara yako ikaendana na
mabadiliko ya kiteknolojia.
Hapa pia naweza kuongeza mtu kukosa maarifa ya kujua jinsi
ya kutumia pesa za biashara yake,kutokujua wapi ni sehemu muhimu ya kutumia
pesa na wapi sio sehemu muhimu. Hili ni jambo la msingi sana kulitambua mana
usipoangalia utabaki kutumia mtaji wote na mwisho wa siku biashara kufa. Kitu
kingine katika matumizi ya pesa usichanganye na matumizi yako binafsi. Lakini
pia nilishawahi kugusia kuhusu vitu ambavyo unatakiwa kutia maanani ili biashara yako
isife mapema unapopata hela katika biashara yako
a. Tenga Malipo Yako
b. Hela ya dharura.
C.Weka Pembeni Kiwango
cha Mtaji wa Biashara Yako.
Hakuna biashara ambayo ni mbaya ila ukikosa maarifa kwasababu unataka kuonekana na wewe unafanya biashara lazima biashara utaiona mbaya.Mtu wa kwanza ambaye ni mbaya katika kuinua biashara yake ni yule ambaye anamiliki biashara na sio biashara yenyewe.
Kusoma makala hizi inaweza isitoshe sana naomba uwasiliane nami uweze kujipatia kitabu changu NGUZO 3 ZA MAISHA sehemu yoyote ulipo kwa 10,000/= na utapata ofa ya kusafirishiwa bure.Kitabu hichi kimeshabadilisha fikra za watu wengi sana ambao napokea shuhuda kutoka kwao na wewe inawezekana huu mwaka kupitia kitabu hiki tukaongea kutengeneza historia ingine.
Ulikuwa nami ;
@Lazaro Samwel
Motivational And Inspirational Speaker
Email ; lazarosamweli41@gmail.com
Contacts ; 0753616584 / 0653386586
0 comments:
Post a Comment