
Habari mpenzi mfuatiliaji wa makala hizi za APPLICATION ya LAZAROSAMWEL namatumaini wiki hii ni wiki ya matunda na wiki ya kukufanya kuwa mpya katika maisha yako.TWENDE PAMOJA kuanza hii wiki salama salmini.
“Haujitengenezei mazingira ila unayachukua mazingira flani kutokana na tabia yako ulivyoijenga. Yani Tengeneza tabia na utachukua mazingira ambayo yanaendana na tabia yako uliyoitengeneza. Ukiwa mvivu utapokea mazingira na matokeo ya kivivu, ukiwa msengenyaji utayachukua mazingira sawa na ulivyo, kila kitu tayari kilishatengenezwa lakini sisi ni kuvichukua tuu kwa tabia zetu. Ni maamuzi yako na sio ya mtu mwingine kwamba unataka vipi? “-Lazaro Samwel
Imam mmoja kwa jina
la Hasan Ali Shah wa Nizari Ismailis aliwahi kusema kwamba “Usimwambie Mungu wako changamoto zako kubwa
kiasi gani,ziambie changamoto zako Mungu wako ni mkubwa kiasi gani”. Nami
ningependa kukwambia kwamba changamoto ambazo huwa tunakutana nazo huwa
tunazivisha sifa ambazo sio katika maisha yetu mpaka zinageuka kuwa matatizo na
kila kukicha tunasahau uwepo wa Mungu mana hata tukiwa tunasali kitu ambacho
kinatawala ni kuombea matatizo na sio kumwomba Mungu kutupa nguvu ya
kuweza kushinda changamoto ambazo tunakutana nazo. Sisi binadamu huwa na mtindo
wa kumwachia Mungu kila kitu tena kwa kurelax na kusema atafanya Mungu, heey,
atafanya endapo na wewe utafanya. Mungu amekupa kila kitu anachohitaji ni wewe
kuvitumia vile alivyokupa, yeye ni kama Mwongozo kwako na kukulinda lakini
tegemeo lake ni kwamba katika kukulinda kwake anategemea wewe kutumia
vile alivyokujalia. Mungu ametuweka katika ulimwengu wenye maarifa, hekima,
mafanikio makubwa n.k hajaweka kulipishwa kodi kuvichukua hivi vitu wala
hajaweza risiti za kupewa baada ya kulipiwa ni wewe mwenyewe tuuu. Kumbuka hata
unavyolalamika kwamba mbona maisha yako hayabadiliki sio kwamba hakuoni anaona
na anakuangalia zaidi atashangaa wewe kutokuvitumia vile alivyokujalia kuwa navyo
licha ya kwamba kutakuwa na changamoto lakini hivyo sio vipaombele katika
maisha yako.
"Mungu
atatengeneza njia pale pasipokuwa na njia" lakini kumbuka hawezi
kutengeneza njia na kukupatia kama wewe mwenyewe hujajiandaa kutembea katika
hiyo njia, hawezi kukutengenezea hiyo njia kama hujajiandaa kihekima na kuwa na
maarifa pamoja na kuwa kiongozi wa wewe mwenyewe. Utashangaa kila siku
unajitahidi sana kusali na kuzungukwa na watu ambao wamefanikiwa lakini bado
njia yako haionekani, sababu inaweza kuwa kwamba kimwili uko na hao watu lakini
ndani yako bado maandalizi ya kukabidhiwa hiyo njia na Mungu bado na Mungu
anakuangalia na kujiuliza lini huyu ataanza kuwa tayari?
Nikirudi mwanzo
katika usemi wa Iman Hasan Ali Shah changamoto ni lazima katika kila jambo
ambalo unalifanya haswa jambo jema, ukiweka katika akili yako na kutambua hili
katika kila jambo ambalo unalifanya Amini hauko mbali katika mafanikio
yako.Cha msingi ni kwamba tusiombee changamoto ila mwombe Mungu wako kuweza
kukupa nguvu za kupambana nazo mana changamoto hata siku moja hauwezi kukwepa
hata Mungu anajua hilo angalia wana wa Israel ambao ni Taifa teule kwa Mungu
walipata changamoto kutoka kwa Wafilistini haijatosha, haijatosha bado walikuwa
watumwa kule Misri kwa miaka zaidi ya 100 walikaa jangwani kwa miaka 40 hizi
zote ni changamoto lakini mwisho wa siku nchi ya AHADI waliweza kuiona.
Unadhani waisrael waliomba kuondokana na changamoto kupitia viongozi wao?
hapana, ila waliomba nguvu ya kuweza kuzishinda.
Muhimu.
Kubali Mungu wako
Akuhamasishe kwanza kabla ya binadamu Kukuhamasisha. Hapo utapata hamasa ya
kwelii ila ukianza na binadamu alafu ikafuata Mungu utakuwa unajidanganya sana.
Na kumbuka Mungu anatengeneza njia pale ambao panaonesha kwamba kunauhitaji wa
kwelii wa hiyo njia, inaweza kuwa njia ya kuwa pastor, mkulima, mfanyabiashara,
mhamasishaji, mwandishi, mfanyabiashara au mjasiriamali,hivi vyote itategemeana
na maandalizi ya tabia zako mana hakuna mabadiliko yoyote ambayo unaweza
kuyapata katika maisha yako bila kubadili tabia kwanza na hakuna mazingira
yoyote mazuri duniani unaweza kuyapata bila kutemgeneza tabia ambayo itavuta
yale mazingira ambayo unayahitaji katika maisha yako.
By LAZARO SAMWEL
CONTACTS : 0753616584 / 0653386586
EMAIL ; lazarosamweli41@gmail.com
FACEBOOK PAGE ; Lazaro Samwel
INSTAGRAM ; Lazaro_samwel3
By LAZARO SAMWEL
CONTACTS : 0753616584 / 0653386586
EMAIL ; lazarosamweli41@gmail.com
FACEBOOK PAGE ; Lazaro Samwel
INSTAGRAM ; Lazaro_samwel3
0 comments:
Post a Comment